Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Issa Mahfoudh Haji, amesema miradi mingi inayotekelezwa ya ujenzi, imekuwa ikikabiliwa na kasoro za manunuzi. Akifungua mafunzo ya siku mbili Kwa maafisa manunuzi wa Ofisi hiyo, amesema tatizo hilo litapata ufumbuzi Kwa kuwajengea uwezo watendaji waweze kuielewa vyema Sheria ya manunuzi.
Amesema uelewa wa Sheria ya manunuzi na uondoshaji wa Mali za umma, iwe ni chanzo muhimu cha kuleta mabadiliko ya kiutendaji.
Akiwasilisha mada ya Sheria ya manunuzi, Mkufunzi Hafidh Rashid, amesema kuwepo Kwa Sheria hiyo kutaimarisha utawala bora, kulinda haki na wajibu, kutatua migogoro ya ununuzi na na kuishauri Serikali kuhusiana na ununuzi. 3/6/2022 ZANZIBAR.
BOFYA HAPA KUPATA TAARIFA KWA NJIA YA VIDEO.