HUDUMA ZINAZOTOLEWA

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ina majukumu makuu yafuatayo:-

  • Kusimamia Sera, Sheria na Kanuni mbali mbali za Ofisi.
  • Kubuni na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo
  • Kudumisha Amani, Ulinzi na Usalama katika Mikoa na Wilaya hadi Shehia.
  • Kulinda mali za Taifa na za watu binafsi zisiharibiwe, kuzuia uingizaji au utoaji nje ya nchi kimagendo, pamoja na kusimamia kazi za uzimaji moto na uokozi.
  • Kuwasajili na kuwapa vitambulisho Wazanzibari wakaazi.
  • Kuwahifadhi kwa kufuata taratibu bora na kwa kuzingatia haki za binaadamu watuhumiwa na waliofungwa ambao wako katika Vyuo vya Mafunzo.
  • Kuandaa na kutekeleza mipango ya kuijengea uwezo Mikoa kitaaluma na utumishi katika Mikoa.
  • Kutoa mwongozo na ushauri kwa Mikoa katika mambo ya kisheria na utaratibu, kujenga mazingira mazuri katika kuimarisha huduma za kijamii na kiuchumi katika Mikoa.
  • Kuratibu, kushauri, kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa shughuliza Serikali za Mitaa.
  • Kuimarisha Utawala Bora na kuimarisha uwezo wa Serikali za Mitaa na mamlaka zake.
  • Kufuatilia na kukagua utendaji wa mamlaka za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ katika utoaji wa huduma.
  • Kuendeleza michezo katika Idara na Taasisi zetu.
  • Kuimarisha uhusiano baina ya taasisi za Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara maalum za SMZ. Na taasisi nyengine.

Wasiliana nasi


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

2277 Barabara ya Vuga,

S.L.P 4220,

70401 Mjini Magharibi,

Tel: +255242230034

Fax: +255242230034

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Waliotembelea Tovuti

3712482
Today
Yesterday
This Week
This Month
All days
41
699
5765
15839
3712482