Waziri wa OR-TMSMIM MH. Masoud Ali Mohammed ameridhishwa na ujenzi wa masoko matatu yanayoendelea kujengwa mkoa wa Kaskazini Unguja.
Ujumbe wa Mameya kutoka Anjouan Visiwa vya Comoro kushiriki katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Serikali za mitaa Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mh Masoud A. Mohammed amewataka wafanyakazi kuzingatia sheria na kanuni za utumishi ili kuepuka kwenda kinyume na miongozo ya kazi inavyo elekeza.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mh Masoud A. Mohammed akagua ujenzi wa Soko la Darajani linalotarajiwa kufunguliwa baada ya wiki moja
Mh. Mudrik Ramadhan Suraga akifungua hafla ya ufunguzi wa kiwanda cha utengenezaji wa Fiber za Kikosi cha Kikosi cha Kuzuia Magendo KMKM
Waziri wa OR-TMSMIM Mhe. Masoud Ali Mohammed, amesema ujenzi wa kituo cha matibabu ya dharura na maabara katika hospitali ya Wilaya Makunduchi, itapunguza masafa ya kufata huduma muhimu nje ya kijiji hicho.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah, amelipongeza Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU) kwa kuwapatia elimu ya ufundi na stadi za maisha vijana, ambao itawawezesha kujitegemea katika maisha yao ya baadae.
Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Hamad Masauni amewatoa hofu wananchi wa Zanzibar kuwa Jeshi la Polisi liko macho katika kupambana na vitendo vya uhalifu, udhalilishaji na masuala yanayowahusu wageni wanaoingia nchini.
Waziri wa OR-TMSMIM Mh. Masoud Ali Mohammed, amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango unaotolewa na vijana wa kujenga Taifa katika ujenzi wa miradi ya Maendeleo hapa nchini.
Waziri wa OR-KSUU Mhe Haroun Ali amesema kufanyika kwa mapinduzi ya mwaka 1964, ni kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kujitawala na kuishi kwa amani na utulivu.
Waziri OR-TMSMIM Mh, Masoud Ali Mohammed akitembelea Jaa la muwekezaji linalokusanya taka za Hotelini katika eneo la Matemwe Wilaya ya Kaskazini ‘A’
Waziri wa Nchi OR - Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Massoud Ali Mohammed amewataka wasimamizi wa ujenzi wa masoko kuhakikisha kuwa ujenzi huo unafanyika kwa haraka kwa vile fedha za uijenzi huo zimeshatolewa.
Waziri wa OR-TMSMIM Mh. Massoud A. Mohammed akifungua mafunzo ya miezi sita ya ushoni kwa wafanyakazi wa Kiwanda cha Idara Maalum za SMZ.
Waziri wa OR-TMSMIM Mh. Massoud A. Mohamed akifungua mafunzo ya kuwawezesha maafisa Mipango wa ORTMSMIM kutafuta fursa za kuwavutia wawekezaji katika maeneo yao.
Kamati ya kusimamia Afisi za Viongozi Wakuu wa Kitaifa ya Baraza la Wawakilishi ilipokuwa ikipokea Ripoti ya utekelezaji wa MIradi ya OR-TMSMIM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mh. Masoud Ali Mohammed akitembelea miradi ya maendeleo katika Shehia ya Fuoni Kipungani na Fuoni Migombani Wilaya ya Magharibi B
Waziri wa Nchi OR - Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Massoud Ali Mohammed amewataka Maafisa wa kikosi cha Zimamoto na Uokozi waliokabidhiwa dhamana kusimamia nidhamu
Waziri OR-TMSMIM Mh. Masoud Ali Mohammed amewataka watendaji wa Manispaa Magharibi A kusimamia vyema vituo vya kukusanyia taka
Waziri OR-TMSMIM Mh. Masoud Ali Mohammed akiwavisha vyeo Maafisa Waandamizi wa Idara Maalum za SMZ
Makamo wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango akiwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa OR-TMSMIM Mh. Massoud A. Mohammed katika Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Nchini Marekani.
Mkurugenzi wa Idara ya Uendeshaji na Utumishi wa OR-TMSMIM akifungua Mafunzo ya mfumo wa E-Office kwa Maafisa Tehama, Utumishi na Masjala kwa Taasisi za OR-TMSMIM yaliyofanyika Vuga Tarehe (9/09/2022)
Ghafla ya utiaji saini kwa Makamanda Wakuu wa Vikosi vya SMZ kuhusu ujenzi wa Masoko Mkoa wa Mjini Magharibi
Ghafla ya utiaji saini kwa Makamanda Wakuu wa Vikosi vya SMZ kuhusu ujenzi wa Masoko Mkoa wa Mjini Magharibi
Makabidhiano ya kazi ya ujenzi wa masoko Mkoa wa Mjini Magharibi kwa Vikosi vya Idara Maalum za SMZ
Makabidhiano ya kazi ya ujenzi wa masoko Mkoa wa Mjini Magharibi kwa Vikosi vya Idara Maalum za SMZ
Makabidhiano ya kazi ya ujenzi wa masoko Mkoa wa Mjini Magharibi kwa Vikosi vya Idara Maalum za SMZ
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mh. Masoud Ali Mohammed Akizungumza na Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad alipokwenda kujitambulisha Ofisini kwake Vuga.
Waziri OR-TMSMIM Mh. Masoud Ali Mohammed, akifungua kikao cha ushirikiano kati ya Wajumbe wa jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania na Wajumbe wa Serikali za Mitaa Zanzibar Ofisini kwake Vuga.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania Nd. Murshid Ngeze akizugumza katika kikao cha ushirikiano kati ya Meya na Wakurugenzi wa Manispaa za Zanzibar na Wajumbe wa Serikali za Mitaa Tanzania.
Mstahiki Meya wa Jiji la Zanzibar, Nd. Mahmoud Mohammed Mussa akifunga kikao cha ushirikiano kati Wajumbe wa Serikali za Mitaa Tanzania Bara na Zanzibar.
Ziara Ya Kutembelea Kazi Za Ujenzi Katika Kambi Nne Za KVZ
Maadhimisho ya siku ya kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya Duniani 26/6/2022 viwanja vya Mapinduzi Square Kisonge Zanzibar.
Maadhimisho ya siku ya kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya Duniani 26/6/2022 viwanja vya Mapinduzi Square Kisonge Zanzibar.
Maadhimisho ya siku ya kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya Duniani 26/6/2022 viwanja vya Mapinduzi Square Kisonge Zanzibar.
VIONGOZI WA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ,WAKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA OFISI HIYO WAKATI WA MAFUNZO KUJENGA UWEZO WA KUZITAMBUA KANUNI ZA UTUMISHI.
VIONGOZI WA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ,WAKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA OFISI HIYO WAKATI WA MAFUNZO KUJENGA UWEZO WA KUZITAMBUA KANUNI ZA UTUMISHI.
VIONGOZI WA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ,WAKIZUNGUMZA NA WATUMISHI WA OFISI HIYO WAKATI WA MAFUNZO KUJENGA UWEZO WA KUZITAMBUA KANUNI ZA UTUMISHI.
WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ, MH. MASOUD ALI MUHAMMED KATIKA PICHA YA PAMOJA NA VIONGOZI NA WATENDAJI WA BARAZA LA MJI KASKAZINI ‘A’ BAADA YA KUMALIZA KIKAO KAZI
Ujumbe wa Waziri

waziripaspotiMnamo Tarehe 19, Novemba 2020 Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi alitangaza Muundo wa Wizara pamoja na Baraza la Mawaziri, ambapo alimteuwa Mheshimiwa Massoud Ali Mohammed (Mwakilishi wa wananchi Jimbo la Ole) kuwa Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ (OR-TMSMIM).

Muundo wa Afisi hii unajumuisha Afisi za Wakuu wa Mikoa, Afisi za Wakuu wa Wilaya, Jiji,  Manispaa, Mabaraza ya Miji na Halmashauri.

Kadhalika Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii, Afisi ya Asasi na Jumuiya zisizokuwa za Serikali (NGO's), Viwanda vya Idara Maalum za SMZ, pamoja na Idara Maalum za SMZ ambazo ni:-

1. Kikosi Maalum Cha Kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM).

2. Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKUZ).

3. Idara ya Chuo cha Mafunzo (MF).

4. Idara ya Zimamoto na Uokozi (KZU).

5. Idara ya Valantia (KVZ).

Aidha kwa mujibu wa ibara ya 123(1) Kamanda Mkuu wa Idara Maalum za SMZ ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Ambapo Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ndie msimamizi wa Afisi inayosimamia Idara Maalum za SMZ.

Katika kutekeleza malengo ya uanzishwaji wa Wizara hii Afisi itahakikisha misingi ya uwajibikaji, uwazi, ufanisi na kujitolea katika ngazi zote za uongozi wa Wizara.

HISTORIA

Kabla ya Mapinduzi ya januari 1964, wananchi walikua hawashirikishwi katika katika maamuzi kuhusu ustawi wa maendeleo yao. Mtiririko wa ngazi za utawala ulikua ni wa kupokea amri na kusimamia utelezaji wa amri hizo ambazo huanzia ngazi ya juu ya...

Soma Zaidi

Dira

Kuwa taasisi imara katika kusimamia amani, usalama, usajili wa wakaazi na upatikanaji wa huduma karibu na wananchi.

 

 

Dhamira

Kujenga mazingira mazuri ya ushiriki wa wananchi katika kudumisha amani ulinzi wa mali zao, kuimarisha huduma za kijamii, kuhakikisha kuwa jamii inashiriki katika kupanga na kusimamia shughuli za maendeleo katika maeneo yao kwa kuzingatia misingi ya utawala bora ikihusisha kuwatambua wakaazi wa maeneo husika na utambulisho wao.

 

Majukumu

Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ ina majukumu makuu yafuatayo:-

  1. Kusimamia Sera, Sheria na Kanuni mbali mbali za Ofisi.
  2. Kubuni na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Soma zaidi

Wasiliana nasi


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

2277 Barabara ya Vuga,

S.L.P 4220,

70401 Mjini Magharibi,

Tel: +255242230034

Fax: +255242230034

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Waliotembelea Tovuti

3605243
Today
Yesterday
This Week
This Month
All days
460
698
2488
3954
3605243