OFISI YA MRAJISI WA JUMUIYA ZISIZO ZA SERIKALI ZANZIBAR

Nini maana ya Jumuiya Zisizo za Kiserikali.

Jumuiya za kiraia ni taasisi binafsi za hiyari zinazoanzishwa kwa lengo la kuiwezesha jamii kushiriki katika shughuli za maendeleo hasa katika maeneo ambayo hayajafanyiwa kazi. Sheria ya Jumuiya No. 6 ya mwaka 1995 ndio inayotumika kuongoza usajili pamoja na kuweka masharti na utaratibu wa usimamizi na uendeshaji wa Jumuiya za hiari.

Aina za Jumuiya za kiraia Jumuiya za kiraia zinaweza kuwekwa katika makundi mbalimbali kutokana na muundo wa Jumuiya, maeneo ya kazi, shughuli inazozifanya au eneo (nchi) la awali ilipoundwa. Jumuiya za kiraia zinaweza kuwa:

  1. Kamati za maendeleo (Community Based Organization – CBOs) hizi ni Jumiya zinazoanzishwa kwa lengo la kufanya kazi katika eneo maalum (lisilozidi wilaya moja)
  2. Za kitaifa (local NGOs) hizi ni taasisi zinazofanya kazi zake ndani ya nchi moja tu.
  3. Za kimataifa (International NGOs) hizi ni zile zinazofanya kazi zake kimataifa (ndani ya nchi zaidi ya moja).

Sifa za Jumuiya zinazosajiliwa Kwa mujibu wa sheria taasisi yoyote inayotaka kusajiliwa kama Jumuiya ya kiraiya Zanzibar ni lazima

  1. Iweni taasisi ya hiyari: kuanzishwa kwake kutokana na hiyari ya waanzilishi wenyewe na kusiwe kwa kulazimishwa ama kutezwa nguvu.
  2. Isijuhusishe na mabo ya kisiasa: kuanzishwa kwa taasisi hakutakiwi kuwe na lengo la kisiasa kama vile kushiriki au kushabikia katika kampeni ya chama Fulani au mgombea Fulani.
  3. Ianzishwe kwa kunufaisha jamii: lengo la kuanzishwa kwake liwe ni kwa maslahi ya jamii inayohusika isiwe kwa maslahi au kutatua matatizo ya mtu binafsi au famulia fulani.

Muda wa kusajili Jumuiya za Kiraia Kwa mujibu wa kifungu nambari 10 cha Sheria ya Jumuiya kila taasisi iliyoanzishwa Zanzibar italazimika kuwasilisha maombi ya usajili kwa Mrajis wa Jumuiya za Kiraia ndani ya siku 28 kuanzia siku ilipoanzishwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa.

Umuhimu wa kusajili Jumuiya za Kiraia Jumuiya za kiraia iliyosajiliwa ina uwezo wa

  1. Kutambulika uwepo wake kisheria
  2. Kupata ruzuku na misaada mengine kiurahisi
  3. Kupata misamaha katika kodi mbalimbali
  4. Kuendesha shughuli zake bila woga
  5. Kuwa na uhusiano mzuri na Serikali pamoja na taasisi nyengine

Matatizo yanayoweza kutokea kwa Jumuiya zisizosajiliwa Jumuiya zisizosajiliwa hukosa

  1. Kutambulika kisheria suala ambalo linaweza kusababisha kukosekana fursa mbalimbali kama vile kuingia katika mikataba.
  2. Uhalali wa uwepo wake husika kisheria.
  3. Fursa ya kufungua akaunti ya Jumuiya.
  4. Fursa ya kutambuliwa kwa taasisi kitaifa na kimataifa na kupelekea kukosa misaada.
  5. Misamaha mbalimbali kwa Serikali mfano msamaha wa kodi n.k

Wajibu wa taasisi iliyosajiliwa

  1. Kuendesha shughuli zake kwa mujibu wa katiba na kanuni.
  2. Kuwasilisha taarifa ya utekelezaji na fedha za kila mwaka kwa Mrajis wa Jumuiya za kiraia.
  3. Kuwa na anuani na afisi inayotambulika.
  4. Kuwasilisha mabadiliko yaliofanywa na taasisi kwa Mrajis.
  5. Kuwa na buku la usajili wa wanachama na mahesabu ya taasisi.
  6. Taasisi inatakiwa iweke utaratibu wa ukaguzi wa mahesabu.

NB. Taasisi yoyote itakayovunjika haitotakiwa kuzigawa mali zinazomilikiwa na taasisi hiyo kwa wanachama wake badala yake i tatakiwa kwa kushirikiana na Mrajis wa Jumuiya za kiraia na mara baada ya kulipa madeni inayodaiwa taasisi hiyo kuzipeleka mali hizo kwa taasisi nyengine, lengo ni kuweza kuendelea kutumika kwa huduma za kijamii.

Fika Ofisi ya Mrajis kusajili Jumuiya na Vielelezo vifuatavyo :-

Kila Jumuiya inapaswa kuwakilisha mambo yafuatayo kwa ajili ya usajili:

  1. Katiba na kanuni za Jumuiya husika
  2. Fomu ya maombi ya usajili itakayokuwa na taarifa za Jumuiya kwa ukamilifu
  3. Orodha ya majina ya wanachama Jumuiya za kigeni zinazotaka kufunguwa tawi Zanzibar

Pamoja na kufuata taratibu zilizotajwa hapo juu pia zitawasilishwa.

  1. Taarifa binafsi (CV) za viongozi wa Jumuiya
  2. Vivuli vya passipoti (kwa wasiokuwa Watanzania)
  3. Kivuli cha kitambulisho kwa Wazanzibari
  4. Kumbukumbu ya kikao kilichoamua kufungua tawi Zanzibar
  5. Barua ya kuteua mwakilishi wa Jumuiya katika usajili wa tawi Zanzibar
  6. Barua ya utambulisho kutoka kutoka Tanzania Bara kwa Jumuiya zinazotaka kuja kufanya kazi Zanzibar.

kwa mawasiliano zaidi wasiliana nasi kupitia anuani zifuatazo:

Ofisi ya RaisTawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

P.O BOX 4220 Vuga - Zanzibar

Tel: +255242230034 Fax: +255242230034

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it. www.tamisemim.go.tz

Wasiliana nasi


Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ

2277 Barabara ya Vuga,

S.L.P 4220,

70401 Mjini Magharibi,

Tel: +255242230034

Fax: +255242230034

Barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Waliotembelea Tovuti

3716302
Today
Yesterday
This Week
This Month
All days
263
71
2501
19659
3716302