Wakulima 135 waliouza zao la miwa msimu huu wakabidhiwa kiasi cha 300,000,000/= kutoka Kiwanda cha Sukari Mahonda Zanzibar, ambapo Chuo cha Mafunzo Zanzibar kimepata hundi ya milioni hamsini (50,000,000/=).
Akikabidhi hundi kwa wakulima binafsi pamoja na Jehi la Kujenga Uchumi JKUZ na Chuo cha Mafunzo Zanzibar, Waziri wa Nchi OR-TAMISEMIM Mhe. Masoud Ali Mohammed amewaomba wananchi kuona umuhimu wa kubadilika na kuzalisha zao la miwa kwani lina tija na soko la uhakika
Aidha amesema uwekezaji wa kiwanda hicho hupeleka kupunguza tatizo la ajira nchini kwa kuimarisha soko la ndani, hivyo ameagiza kwa Idara Maalum za SMZ kujitathmini na kuangalia uwezekano wa kuyatumia maeneo ya kilimo kwa kuimarisha wakulima wa miwa.
BOFYA HAPA KUPATA TAARIFA KWA NJIA YA VIDEO.
|
|